Psalms 14:1-3

Uovu Wa Wanadamu

(Zaburi 53)

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Mahalathi. Zaburi Ya Daudi)


1 aMpumbavu anasema moyoni mwake,
“Hakuna Mungu.”
Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa;
hakuna hata mmoja atendaye mema.


2 b Bwana anawachungulia wanadamu chini
kutoka mbinguni
aone kama wako wenye akili,
wowote wanaomtafuta Mungu.

3 cWote wamepotoka,
wameharibika wote pamoja,
hakuna atendaye mema.
Naam, hakuna hata mmoja!

Copyright information for SwhKC